IBADA YA KINABII MAHALI ULIPO.
KILA SIKU YA ALHAMISI MUDA KUANZA SAA 2:00 USIKU HADI SAA 4:00 USIKU.
Kutokana Na Uhitaji Wa Watu wengi Kwenye Mtandao Wa HUDUMA YA MLANGO WA UKOMBOZI, Tumeanzisha Maombi Ya KUFUNGA Kila Siku Ya ALHAMISI Ya Kila Wiki.
Kila Mshirika Wa Huduma Hii atawajibika Kuzingatia Yafuatayo.
1.kufunga Masaa 12
2.kutuma Mahitaji Yake Siku Moja Kabla Ya Maombi Kwenye Group la Huduma.
3. Kuanza Maombi Ya Kuombea Mahitaji Kwa Watu wote MUDA Kuanzia Saa 2:00 USIKU Hadi Saa 4:00 USIKU.
4. Hakikisha Unaombea Mahitaji Ya Watu na Yako Pia Kwa Pamoja.
5. Maombi Haya Yataongozwa Na Nabii Kiongozi Wa Huduma Kwa Muda Husika
6. Hii itakua ni IBADA Kama Ibada Zingine Tunazozifanya Tofauti Yake Ni Ibada Itakayofanyika Kila Mtu Akiwa Nyumbani Kwake. Hivyo ni Ibada Itakayoambatana Na SADAKA Siku Ya Huduma
7. Kila Wiki Kabla Ya Maombi Litatumwa Neno La Kusimamia Kwa Ajili Yako Kuomba.
8. Ibada Hii Itawahusu Watu waliokwenye MTANDAO TU wanaotoka Mbali Na Eneo Letu la Huduma.
9. Hakikisha Muda Huo Uliopangwa Unakua Nyumbani Kwako Na Umeanza Maombi.
10. Nabii Ataongoza Ibada Hii Ya KINABII Kwa Masaa Hayo
MUHIMU.
KUHUSU DK 30 ZA KUPOKEA MUHUJIZA.
Kuanzia SAA 2:00 Hadi Saa 2:30 Hizi Zitakuwa ni DK 30 Za KUGUSA SIMU NA KUPOKEA MUHUJIZA WAKO. HIVYO Hakikisha UNAGUSA SIMU YAKO, Utaweka Simu Yako Kiganjani Kwenye SCREEN kisha Utulie Nabii Atakua Anakuombea Kwa Muda Huo.
Zingatia,. HII Ni IBADA YA AJABU SANA KWAKO WATAKAO AMINI WATAPOKEA KWA ISHARA, AJABU NA MIHUJIZA.
KAMA UMEPOKEA UJUMBE HUU SEMA AMEN.
Kisha Tuma Mahitaji Yako KAMA Unaona Kuna MAHITAJI Ya SIRI huwezi KUTUMA Kwa GROUP Nitumie Private Kwenye Inbox.
NENO LA KUSIMAMIA WIKI HII
YEREMIA 31:21-22
BWANA ATAFANYA JAMBO JIPYA KWAKO LEO
BARIKIWA
Na Nabii.E.M Thadeo
MLANGO WA UKOMBOZI MINISTRY.
Founder.
April 2016
IBADA YA KINABII MAHALI ULIPO.
KILA SIKU YA ALHAMISI MUDA KUANZA SAA 2:30 USIKU HADI SAA 4:00USIKU.
Kutokana Na Uhitaji Wa Watu wengi Kwenye Mtandao Wa HUDUMA YA MLANGO WA UKOMBOZI, Tumeanzisha Maombi Ya KUFUNGA Kila Siku Ya Alhamisi Ya Kila Wiki.
Kila Mshirika Wa Huduma Hii atawajibika Kuzingatia Yafuatayo.
1.kufunga Masaa 12
2.kutuma Mahitaji Yake Siku Moja Kabla Ya Maombi Kwenye Group la Huduma.
3. Kuanza Maombi Ya Kuombea Mahitaji Kwa Watu wote MUDA Kuanzia Saa 2:30 USIKU Hadi Saa 4:00 USIKU.
4. Hakikisha Unaombea Mahitaji Ya Watu na Yako Pia Kwa Pamoja.
5. Maombi Haya Yataongozwa Na Nabii Kiongozi Wa Huduma Kwa Muda Husika
6. Hii itakua ni IBADA Kama Ibada Zingine Tunazozifanya Tofauti Yake Ni Ibada Itakayofanyika Kila Mtu Akiwa Nyumbani Kwake. Hivyo ni Ibada Itakayoambatana Na SADAKA Siku Ya Huduma
7. Kila Wiki Kabla Ya Maombi Litatumwa Neno La Kusimamia Kwa Ajili Yako Kuomba.
8. Ibada Hii Itawahusu Watu waliokwenye MTANDAO TU wanaotoka Mbali Na Eneo Letu la Huduma.
9. Hakikisha Muda Huo Uliopangwa Unakua Nyumbani Kwako Na Umeanza Maombi.
10. Nabii Ataongoza Ibada Hii Ya KINABII Kwa Masaa Hayo
MUHIMU. KUHUSU DK 30 ZA KUPOKEA MUHUJIZA.
Kuanzia SAA 2:30 Hadi Saa 3:30 Hizi Zitakuwa ni DK 30 Za KUGUSA SIMU NA KUPOKEA MUHUJIZA WAKO. HIVYO Hakikisha UNAGUSA SIMU YAKO, Utaweka Simu Yako Kiganjani Kwenye SCREEN kisha Utulie Nabii Atakua Anakuombea Kwa Muda Huo.
Zingatia,. HII Ni IBADA YA AJABU SANA KWAKO WATAKAO AMINI WATAPOKEA KWA ISHARA, AJABU NA MIHUJIZA.
KAMA UMEPOKEA UJUMBE HUU SEMA AMEN.
Kisha Tuma Mahitaji Yako KAMA Unaona Kuna MAHITAJI Ya SIRI huwezi KUTUMA Kwa GROUP Nitumie Private Kwenye Inbox.
NENO LA KUSIMAMIA WIKI HII
LUKA 17:7-8
BWANA KUKUPATIA HAKI YAKO UPESI
BARIKIWA
Na Nabii.E.M Thadeo
MLANGO WA UKOMBOZI MINISTRY.
Founder.
April 2016
MAOMBI 2016
MUONGOZO WA
MAOMBI YA MFUNGO WA SIKU 30 KUOMBEA HUDUMA ZOTEZITAKAZOFANYIKA MWAKA 2016
MAOMBI HAYA YATAANZA TAREHE
10.01.2016 HADI 10.02.2016.
KICHWA CHA MAOMBI SOMO NI
KUTOKA ISAYA˸ 60˸ 1-6
BWANA YESU KUTUZUKIA NA
UTUKUFU WAKE KUONEKANA JUU YA HUDUMA
UTANGULIZI÷
Tunamshukuru sana Mungu kwa mara nyingine kutupatia nafasi nyeti na
muhimu sana ya kuendelea na maombi haya. Huu ni mfululizo wa maombi ya kila mwaka
ambayo hufanyika mwanzoni mwa mwaka. Maombi haya yametuwezesha kwa kiwango
kikubwa kuinuua huduma hii na kupitia
Maombi haya tumepata mafanikio makubwa ya kihuduma.
Huu ni mwaka wanne tangu Bwana Yesu aliponipa maono haya 2011, na timu
ya Huduma ya MLANO WA UKOMBOZI
ikiongozwa na Nabii E.M Thadeo
inashiriki maombi haya kwa mara ya pili baada ya kuamza Huduma hii mwaka 2014.
Kwa pamoja tunashiriki katika kuhakikisha tunafunga kwa kipindi chote
cha siku 30 kwa maombi ya saa 12 tukilia na Bwana juu ya huduma hii.
MWONGOZO WA MAOMBI YA TOBA (MATENDO
YA MITUME 3˸ 17-21)
Neno linasema tubuni basi mrejee ili dhambi zenu zifutwezipate kuja
nyakati za kuburudishwa na Bwana
Ø Ndani ya toba kuna msamaha na Kuburudishwa
hakika
Ø Katika hatua hii lazima uzame katika toba
ili Bwana aweze kuachilia na kututoa katika vifungo , uburudishwe na Bwana
Yesu.
Ø Achilia toba kwenye familia yako,
ndoa,ukoo, nchi yetu
Ø Raana za Ukoo,maagano yaliyofanyika juu
yako,
2.
BWANA YESU KUTUZUKIA NA UTUKUFU WAKE KUONEKANA JUU YA HUDUMA (ISAYA 60˸1 -6)
Bwana alinisemesha juu ya
neno hili mwaka huu ya
kuwa ni saa ya KUONDOKA na KUANGAZA kwani nuru ya Kristo inakuja.
Ni mwaka wa huduma ya MLANGO WA
UKOMBOZI Kuondoka na kuangaza katika mataifa yote duniani. Katika ombi hili
shughulika na mambo yafuatayo
Ø Nuru ya Huduma ing'ae sasa katika mataifa
yote.
Ø Utukufu wa Bwana uje juu ya Huduma hii
Ø Mataifa kujia Nuru ya MLANGO WA UKOMBOZI
Ø Mataifa watakuja na wafalme wao kutokana
na kuzuka kwa utukufu wa Bwana
Ø Watakusanyana waje kwenye MLANGO WA UKOMBOZI -watu wengi
kama bahari
Ø Baba ainue wana kutoka mbali watakuja LANGONI
Ø Utajiri wa mataifa utakuja katika Huduma
HII
Ø Watu watakuja kutoka kila pande (kusi na sheba)
wataleta dhahabu kwa Bwana
Ø Sifa za Bwana zitatangazwa kupitia hii madhabahu ya MLANGO WA UKOMBOZI
Ø Litafanyika Lango la makimbilio kwa
mataifa yote
3.
MAOMBI YA KUTEKA, KUPIGA, KUTEKETEZA FALME ZA KUZIMU ZINAZOZUIA HUDUMA HII ISAYA 8˸11-15
- MAOMBI YA KUFANYA MATEKA
Mathayo 11˸12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa
ufalme wa Mbinguni unatekwa na wenye nguvu. Anza kuteka ufalme wa Mungu na
kuteka nguvu za giza zifanye mateka Kutoka
12˸ 36- Bwana aliwawezesha wana wa Israeli kuwateka Wamisri nyara.
·
Anza
kuteka nyara falme zinazozuia Huduma
·
Teka
ngome za kichawi na KIganga
·
Teka
fikra za watu wanaohudhuria maombi ya Ibada
za Kinabii waelewe mafundisho, watamani kukaa LANGONI Siku zote, wasiondoke kabisa, hata wakielezwa maneno ya
Uzushi wasiyasadiki.
·
Fanya
mateka kila roho inayoangamiza huduma.
·
Fanya
mateka nguvu za kuzimu Madhabu za
Rusifer na nguvu zozote za kuzimu.
·
Fanya
mateka Maeneo tunayofanyia Huduma zetu
·
Fanya
mateka anga,ardhi, bahari na kuzimu
II.
MAOMBI YA KUPIGA FALME –Kutoka 12-29;
Kumb 20˸ 1-4
Usiku wa manane Bwana akawapiga wazaliwa
wa kwanza wa nchi yote katika Misri-kile kipigo kilisababisha Farao awape
Ruhusa wana wa Israeli wakamtumikie Mungu wao.
Zipige falme zote za kipepo,kichawi,kuzimu,
madhabahu za kishetani na nguvu zote ulizoziteka
hapo juu.
III
MAOMBI YA KUTEKETEZA NA KUANGAMIZA˸ Yer 1˸ 4-10, Kutoka 23˸ 24
Bwana anamwambia Musa yakuwa asisujudie
miungu yao bali aiangamize kabisa na kuzivunja nguzo zao. Pia DANIEL 8˸ 24
·
Angamiza
kila aina ya ufalme uliouteka hapo juu
·
Hakikisha
unateketeza kabisa kila hila za adui juu ya huduma zisiinuke tena hizo nguvu za
adui.
4. MAOMBI YA KUACHILIA ISHARA, MIUJIZA NA
MAAJABU JUU YA MADHABAHU YA MLANGO WA UKOMOZI ( Yoshua 3˸ 5-7, Zab 77˸ 14, Zab
136˸4)
A.
Bwana akamwambia Yoshua waambie watu wajitakase maana Bwana atatenda mambo ya
ajabu kati yao. Yoshua akaliinua sanduku la agano Bwana akamtukuza mbele ya
Israeli wote.
Kama vile Bwana alivyoonekana kwa Musa na Yoshua vivyo hivyo Bwana akaonekane kwetu kwa kiwango hicho hicho
cha ishara na maajabukatika huduma hii.
Marko
16˸ 17 Yesu alisema na
ishara hizi zitafuatana nao. Bwana aachilie ishara juu ya Huduma
Kutoka
34˸ 10 – Bwana alisema
mbele ya watu wangu wote mtatenda miujiza ya namna isiyotendeka katika dunia
yote wala katika taifa lolote na watu wote unaokaa kati yao.
Matendo
19˸11- Mungu akafanya kwa
mikono ya Paulo miujiza ya kupita
kawaida.
Ni wakati wa MADHABAHU YA MLANGO WA UKOMBOZI kutenda miujiza mikubwa kupita
kawaida
§
Magonjwa
ya kila aina kuondoka juu ya watu watakaokanyaga katika madhabahu hii.
§
Pepo
wachafu wa kila aina kuwatoka watu kabisa na kuachwa huru
§
Tabiri
viziwi, viwete, vipofu,waliovunjika viungo,kansa,waliopooza, waliochukuliwa
misukule,waliopotea na kila aina ya vifungo ni saa yao kupitia madhabahu hii
kufunguliwa.
B.
Maombi ya kuvunja roho za uharibifu , kuchafua, kukashifu, kupinga Madhabahu
hii, zuia vifo, kafara, kudhalilishwa,kuteswa juu ya Hii Madhabahu.
katika Ombi hili hakikisha unaomba vitu
vifuatavyo˸
·
Hakikisha
unashughulikia kila roho ya Uhalibifu wa vyombo vya huduma na uharibifu wowote
·
Vunja
roho za Kuchafua huduma kwa Maneno ya watu
·
Vunja
roho za kukashifu huduma hii kwa watu
·
Roho
za kupinga Madhabahu hii na kazi zote zinazofanyika hapa
·
Zuia
roho za vifo kwa watu wanaokuja kuhudumiwa kwenye hii Madhabahu hii na vifo vyovyote vya
Watumishi katika Huduma hii.
·
Vunja
roho za Mafarakano kwa Watumishi na Ndoa zao kisha wanaohudumiwa wasifarakane
baada ya huduma
·
Kataa
kila roho za udharirishaji wa aina yoyote juu ya Madhabahu n watumishi,na watu
wote
·
Kataa
roho za Mateso ya kila aina juu ya Madhabahu na watumishi wake.
·
Yafute
maneno Yote yaliyotamkwa juu ya Hii Madhabahu.
C.
Maombi ya kuachilia moto juu ya madhabahu ya mlango wa ukombozi
na
watumishi wake wote.
Walawi
6˸8-13- Bwana alisema na Musa juu ya moto wa kuteketeza sadaka
kuwa moto wa madhabahuni utatunzwa uwake daima
juu ya ile madhabahu wala wala
usizimike daima
Ebrania
12˸29 Yesu kristo ni moto
ulao
Achilia moto wa kristo ulao uwake katika
madhabahu na watumishi wake usiku na mchana ukateketeze kila falme na nguvu za
adui
Achilia nguvu ya upako kwa moto katika
madhabahu.
5. MAOMBI YA KUMUOMBEA NABII E.M.
THADEO-MBEBA MAONO JUU YA HUDUMA HII ANAZOZIFANYA (ISAYA 22˸20-25)
ISAYA
22˸20-25- Bwana akasema
nitamwita mtumishi wangu Eliakimu
namI nitamvika vasi lako (Isaya) nitamtia nguvu nitamkabidhi mamlaka yako
atakuwa Baba wa wenyeji wa Yerusalemu. Omba Bwana aachilie vitu vifuatavyo kwa
Nabii
Ø
Amvike
vazi la kinabii juu ya Huduma
Ø
Amtie
nguvu katika huduma zote kwa mwaka mzima
Ø
Ampe mamlaka ya kuukumu Falme na Mamlka za
Kuzimu.
Ø
Baba ampe funguo kama alivyompa Daudi,
mamlaka yawe juu ya Nabii wakati wa wote( atafunga hakuna atakayefungua)
Ø
Amfanye
Kiti cha utukufu katika mataifa yote
Ø
Awe imara kama msumari uliokazwa bila
kutetereka katika kipindi chote cha Huduma
( Nguzo ya chuma)
Ø
Baba
wa Mbinguni ampe kuketi katika Kiti
cha Huduma
A. Bwana kuachilia maono makubwa zaidi juu ya Huduma
YOEL 2˸ 28-30 Bwana akamimine Roho wake
juu ya maono Huduma tunazozifanya
B. Ampake mafuta zaidi ya aliyompaka Daudi
Mtumishi wake Zab 89˸20
C.
Ampe
utiisho na Kuhofiwa kwa kiwango kikuu
Kumb 11˸20 -25
6. MAOMBI YA KUOMBEA WATUMISHI NA HUDUMA
ZITAKAZOFANYIKA MWAKA JAN-DEC 2016
A).
WATUMISHI, Mwambie Bwana
Yesu asimamishe watumishi watakaotumika katika madhabahu hii kwa UAMINIFU Katika kipindi chote cha
Huduma
Ø
Wapake
mafuta ya utumishi Zab 89˸20
Ø
1Nyakati 28˸9 Watakaotumika kwa moyo wa ukamilifu
Ø
Galatia 5˸13 Watakaotumika kwa Moyo wa Upendo
Ø
1 Samwel 12˸14-15 Watakaoisikia sauti ya Kristo katika
utumishi wao
Ø
Yeremia 51˸ 20-24 Bwana awafanye Rungu la Silaha za Kivita
Ø
Isaya 39˸29-31 Wenye nguvu mpya kila siku wasiochoka
usiku na mchana katika Huduma
Ø
Watumishi
wote watapakwa mafuta aliyopaka mafuta Nabii
Kiongozi ili waweze kutumika kikamilifu katika huduma zote
Ø
Adui
hatawashinda katika hududma (wasioshindwa na kitu chochote katika huduma na utumishi
wao
Ø
Baba
wa mbinguni awape heshima Yohana 12˸26
Mtu akimtumikia BABA wa mbinguni atakuheshimu ndoa, fedha, magonjwa n.k
7.
KUOMBEA MIPANGO NA HUDUMA ZITAKAZOFANYIKA MWAKA 2016
I.MIPANGO
Ø
Kufungua
TOVUTI ya Huduma
Ø
Kununua
viwanja Ekari 20 katika eneo la huduma
Ø
Kujenga
Hema la maombi ukumbi wa kupokea watu 1000
Ø
Ujenzi
wa shule kama kitega Uchumi cha Huduma
Ø
Kununua
vyombo vya muziki vya kutosha
Ø
Kununua
Viti vya kutosha watu 500
Ø
Kukamilisha
usajili wa Huduma wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Ø
Kuanzisha
Mradi mbalimbali ya huduma utakaowezesha huduma kukua
Ø
Kununua
Gari la huduma
Ø
Ujenzi
wa Miundombinu ya huduma
Ø
Kufanya
huduma katika mikoa yote Tanzania bara na Visiwani na Duniani
Ø
Kuinua
waratibu wa Huduma katika mikoa yote na Duniani
Ø
Kuwahudumia
wajane,Yatima na wasiojiweza kikamilifu na kuanzisha siku za wajane na Yatima
kwa kukaa pamoja.
II.HUDUMA ZOTE
Ø
Ibada
za kinabii za ukombozi Jumamosi na Alhamisi- Prophetic services
Ø
Kuanzisha
Ibada za uponyaji-Jumanne
Ø
Huduma
zote za mikoani na safari zote
Ø
Huduma
za MAJI YA UFUFUO NA UZIMA
Ø
Maombi
ya kugusa TUFE LA RAMANI YA DUNIA
kuita waumini kutoka Dunia kote waje kwenye Madhabahu hii.
ZINGATIA÷ Ni wakati wa huduma kung'aa
na wanaokuja watatamani kukaa hapa kumwabudu mungu marko 9˸2-7
8. KUINUA WATU WATAKAOTEGEMEZA HUDUMA KWA FEDHA NA WAOMBAJI
(G.R.M PARTINERS)
Isaya 60˸6 ( b) Zab 72˸10, Mathayo 2˸11
Bwana alisema toka Kushi
na Seba na mataifa yote watakuja wataleta
dhahabu na uvumba na kuzitangaza sifa za Bwana na kufungua hazina zao .
katika hatua hii kutokana na huduma kuwa na Mahitaji mengi huku uwezo wetu
kiuchumi kuwa mdogo lazima tumwombe Bwana Yesu kwa mzigo alete watu
watakaomtumikia Mungu kwa fedha zao zitakazosaidia kuinua huduma.
Tamka yafuatayo÷
Ø Waite waje kutoka pande nne za dunia
Ø Wafungulie milango ya
fedha
Ø Achilia kiu yao juu ya
kutoa kila walichonacho kwa Bwana juu ya madhabahu hii
Ø Vunja roho ya kukaidi
maelekezo ya Roho Mtakatifu kwa kile Mungu atawasemesha watoe
Ø Omba watoe vitu kamili
sio vilema au vitu visivyofaakatika madhabahu
Ø Vunja nguvu za shetani
zinazowazuiya watu wasitoe vitu vyao walivyonavyo katika madhabahu hii
Ø Wapande watu hao
watakaotegemeza huduma katika madhabahu
WAOMBAJI KUOMBEA MADHABAHU HII KUTOKA NJE
Ø Waite waombaji kutoka
pande zote watakaotegemeza na huduma hii Kwa njia ya Maombi
Ø Achilia Roho ya kila
anayekanyaga katika hii madhabahu kuombea hii madhabahu
Ø Bwana awainue waombaji
wasiochoka
Ø Wasionyamaza kila siku
Ø Na kila Mwombaji
atakayeiombea Madhabahu hii abarikiwe kwa kiwngo kikuu na Mungu amuinue.
9. MAOMBI YA KUOMBEA MJI WA GAIRO, TAIFA LETU NA TAIFA LA ISRAELI
Zab 122˸6, Yeremia 29˸7
Neno linasema utakieni Yerusalemu
amani na wafanikiwe wakupendao. Pia utakieni amani mji ule ambao mmechukuliwa
mateka, mkauombee kwa Bwana kwa maana katika
amani yake huo mji ninyi mtapata amani.
MJI WAGAIRO
Katika maombi haya lazima
tuombee mji tuliopo Gairo na kisha
tuuteke na kuumiliki wote sisi tukawe watawala wala hakuna mwingine.
Tutazunguka Mji wote na kuutwaa kuwa mateka yetu.
Waamuzi 5˸12 Amka uwachukue mateka, ni saa ya kuchukua Gairo mateka na vitu vyake vyote ili tuumiliki.
Yoshua 8˸1-9 Bwana anautia mji wa Ai
mikononi mwa mfalme. Hivyo hivyo Bwana lazima autie Gairo na viunga vyake vyote mikononi mwetu hakika.
TAIFA LA TANZANIA
Ø Amani juu ya nch yetu( Zab 122˸8)
Ø Raisi John Pombe Magufuli
kutawala nchi. Pinga roho za upinzani juu yake, vifo, mikosi na balaa juu yake,
mfiche kwa Damu Ya Yesu.
Ø Omba toba juu ya maasi
yote yanayotendeka umwagaji damu wa
ajali zisizoisha 1 Thesalonike 5˸23
Ø Zuia roho za vita vya
aina yoyote katika nchi yetu
Ø Agiza haki juu ya taifa letu Isaya 61˸11
TAIFA LA ISRAELI
Ø Kulinda Taifa la Israeli
na roho za adui
Ø Watu wa Taifa hili watoke
katika huzuni na machozi wanayolia
Ø Kuombea wenyeji wa
Yerusalemu ambao wameishi kwa shida siku nyingi Bwana awafariji
Ø Zuia mapambano ya vikundi
vya ugaidi katika Yerusalemu
Ø Bwana ashughulike na
wanaoiletea hofu Israeli kutoka Mashariki ya Kati
Ø Tumuombee waziri mkuu wa
Taifa la Israeli
Ø Silaha zote zilizoinuka
juu ya Israeli zisifanikiwe
Ø Futa matamko, laana,
mikosi juu ya Taifa zisifanikiwe
Ø Taifa la Israeli wapokee
wokovu Isaya 62˸11
10. MAOMBI YA ULINZI NA SHURANI
KWA BWANA
A. MAOMBI YA ULINZI.
Zab 66˸9, Mathayo 10˸29
Omba
ulinzi toka kwa KristoYesu yeye amesema
hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote hivyo tusiogope hata kidogo nguvu
za adui hazitatushinda, pia alisema hakuacha mguu wetu usogezwe hata kidogo
Ø Matendo 17˸28 Ndani ya Kristo tunaishi tunakwenda na kuwa na uhai wetu
Ø 1 Samweli 25˸29 Hata kama binadamu akiinuka bado nafsi zetu zingefungwa kwenye uhai
pamoja na kristo Yesu
Ø Bwana afiche huduma zote
tunazozofanya
Ø Ulinzi juu ya familia
zetu
Ø Ulinzi juu ya roho ya
visasi kutoka kwa adui
Ø Uhai wa watumishi ulinzi
hasa katika magonjwa hakuna kuumwa kwa watumishi na familia zao zote
Ø Kila tutakapokanyaga
kwenye huduma tulindwe hakika
Ø Tufichwe tusionekane
sisi, watoto,ukoo, ndoa kwa damu ya Yesu
Ø Vyombo vya usafiri
vyovyote tunavyitumia kila siku
Ø Vyombo vya huduma kama
spika,genereta,viti na vifaa vyote vya huduma vilindwe
Ø Zuia ajali, kafara na vifo
kwa watumishi katika huduma na watu tunaowahudumia hakuna vifo juu yao
Ø Ulinzi juu ya mali zote
kama mashamba, ofisi na mali za ofisi
Ø Kataa kabisa Roho ya Vifo
na kafara kwenye Madhabahu Hii
B. MAOMBI YA SHUKRANI
Isaya 12˸1, 1wakorinto 15˸57
Ø Tunamshukuru sana Bwana
Yesu kwa kuachilia maono haya juu ya huduma kwa kipindi chote cha huduma mahali
hapa tumetiwa nguvu za ushindi mkuu.
Ø Ashukuriwe atupaye
kushinda 1 wako 15˸57
Maombi haya Yameandaliwa na
Nabii E.M.Thadeo.
HUDUMA YA MLANGO WA UKOMBOZI
Dec. 2015
No comments:
Post a Comment